Yale tunayoyawaza na kuyatafakari kwenye fikra zetu yana nafasi kubwa sana kwenye maisha yetu. Ikiwa tunataka kufanikiwa basi ni lazima tufikiri na kutafakari juu ya kufanikiwa.
“Tunakuwa kile tunachofikiri”
Earl Nightingale
Vivyo hivyo ikiwa tunahitaji kuhamasika kufanya mambo mbalimbali maishani, ni lazima tusome, tusikilize, tutazame na hata tutafakari vitu vitakavyotuhamasisha.
Karibu nikufahamishe nukuu 50 (quotes) ambazo zitakuhamasisha katika maswala mbalimbali unayoyafanya maishani mwako.
1.
“Chochote ambacho akili ya binadamu inaweza kuumba na kufikiri, inaweza kukikamilisha pia.”
Napoleon Hill
2.
“Njia ya kuanza ni kuacha kuzungumza na kuanza kutenda.”
Walt Disney
3.
“Usiruhusu jana itawale sana leo.”
Will Rogers
4.
“Kama unafanyia kazi kitu kinachokusisimua na unachokijali kweli, hauhitaji kusukumwa. Maono yako yatakusukuma.”
Steve Jobs
5.
“Kufahamu haitoshi, ni lazima tuweke kwenye matendo, Kutamani haitoshi, ni lazima tufanye.”
Johann Wolfgang
6.
“Tunatengeneza hofu tunapokaa bila kufanya kitu. Tunaishinda hofu kwa matendo.”
Dr. Henry Link
7.
“Ikiwa unafikiri unaweza au huwezi, uko sahihi.”
Henry Ford
8.
“Mtu mwenye kujiamini ndani yake, anapata kujiamini kwa wengine.”
Hasidic Proverb
9.
“Fanya kile unachoweza kwa vyote ulivyonavyo, popote ulipo.”
Theodore Roosevelt
10.
“Akili ni kila kitu. Unavyofikiri ndivyo unavyokuwa.”
Buddha
11.
“Muda mzuri wa kupanda mti ni miaka 20 iliyopita. Lakini muda mwingine mzuri wa pili ni sasa.”
Chinese Proverb
12.
“Muda wako ni mdogo, usiupoteze kuishi maisha ya mtu mwingine.”
Steven Jobs
13.
“Kushinda siyo kila kitu, lakini kutaka kushinda ni kila kitu.”
Vince Lombardi
14.
“Huwezi kuvuka bahari kama huna ujasiri wa kuacha kuona ufukwe.”
Christopher Columbus
15.
“Kisasi kizuri ni mafanikio makubwa.”
Frank Sinatra
16.
“Kuna njia moja tu ya kuepuka kukosolewa: usifanye kitu, usiseme kitu na usiwe chochote.”
Aristotle
17.
“Anzia ulipo. Tumia kile ulichonacho. Fanya kile unachokiweza.”
Arthur Ashe
18.
“Anguka mara saba simama mara ya nane.”
Japanese Proverb
19.
“Mlango mmoja wa furaha ukifungwa, mwingine unafunguliwa, lakini mara nyingi tunautazama sana ule uliofungwa na kushindwa kuona ule uliofunguliwa kwa ajili yetu.”
Helen Keller
20.
“Kila kitu kina uzuri wake, lakini siyo kila mtu anaweza kuuona.”
Confucius
21.
“Changamoto zinafanya maisha yavutie na kuzishinda ni kufanya maisha kuwa na maana.”
Joshua J. Marine
22.
“Kama unataka kujiinua mwenyewe juu, mwinue mwingine juu kwanza.”
Booker T. Washington
23.
“Ili kufanikiwa, shauku yako ya mafanikio ni lazima iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.”
Bill Cosby
24.
“Kila siku ninajitahidi kufanya vizuri zaidi kuliko nilivyo fanya jana.”
Reginald Mengi
25.
“Mtu ambaye hajawahi kufanya kosa hajawahi kujaribu kitu chochote.”
Albert Einstein
26.
“Mtu anayesema hawezi kufanya hatakiwi kumwingilia mtu anayesema ninaweza kufanya.”
Chinese Proverb
27.
“Haujachelewa kuwa ambaye ungeweza kuwa.”
George Eliot
28.
“Unakuwa kile unachoamini.”
Oprah Winfrey
29.
“Jenga ndoto zako wewe mwenyewe, la sivyo mtu mwingine atakuajiri kujenga zake.”
Farrah Gray
30.
“Ota ndoto kubwa na dhubutu kushindwa”
Norman Vaughan
31.
“Badili kufikiri kwako na utakuwa umebadili ulimwengu.”
Norman Vincent Peale
32.
“Andika kitu chenye manufaa kusomwa au fanya kitu chenye manufaa kuandikwa.”
Benjamin Franklin
33.
“Njia pekee ya kufanya kazi nzuri ni kupenda kile unachokifanya.”
Steve Jobs
34.
“Ikiwa unaweza kuliota, unaweza kulifanikisha.”
Zig Ziglar
35.
“Ndoto zetu zote zinaweza kutokea ikiwa tuna ujasiri wa kuzifuata.”
Wale Disney
36.
“Usilie juu ya kile ambacho huna; tumia vizuri kile ulichonacho.”
Reginald Mengi
37.
“Mambo mazuri huja kwa watu wanaosubiri, lakini mambo bora huja kwa wale wanaoondoka na kwenda kuayachukua.”
Hajulikani
38.
“Fursa hazitatokea, unatakiwa kuziunda.”
Chris Grosser
39.
“Usijaribu kuwa mtu wa mafanikio, bali jaribu kuwa mtu wa thamani.”
Albert Einstein
40.
“Akili kubwa hujadili mawazo, akili ya wastani hujadili matukio, akili ndogo huzungumzia watu.”
Eleanor Roosevelt
41.
“Ikiwa hauthamini muda wako, hata wengine hawatauthamini. Acha kupoteza muda na vipaji vyako sasa – anza kuvifanyia kazi”
Kim Garst
42.
“Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na wengine.”
David Brinkley
43.
“Usiinue sauti yako, boresha hoja yako.”
Hajulikani
44.
“Ninaamini kwamba ujasiri pekee mtu yeyote anaouhitaji ni ujasiri wa kufuata ndoto zako mwenyewe.”
Orarah Winfrey
45.
“Fursa zina aibu, zinakusubiri uzikimbilie.”
Reginald Mengi
46.
“Ubunifu unatofautisha kati ya kiongozi na mfuasi.”
Steve Jobs
47.
“Hofu ni mojawapo ya adui mkubwa kwa mafanikio.”
Reginald Mengi
48.
“Wengi wetu hatuishi ndoto zetu kwa sababu tunaishi hofu zetu.”
Less Brown
49.
“Hatua ya mwanzo ya mafanikio yoyote ni matamanio.”
Napoleon Hill
50.
“Baadaye inamilikiwa na wale wote wanaoamini kwenye uzuri wa ndoto zao.”
Eleanor Roosevelt
Naamini umehamasika na kufurahia nukuu hizi za hamasa. Ni wazi kuwa kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu – tunavyowaza ndivyo tunavyokuwa.
No comments:
Post a Comment